This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/03/28 at 22:46
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Chama cha Mapinduzi (CCM) ni muungano baina ya Tanganyika African National Union (TANU)  na Afro- Shirazi Party  (ASP), Vyama viwili vya siasa vilivyoongoza harakati za kupigania  uhuru wa Tanzania  bara na Zanzibar , mtawalia. Vyama hivyo viliungana tarehe 5 Februari, 1977. 

Hivi sasa CCM inamiliki  UHURU Media Group (UNG) yenye uhuru  Publications  Limited (UPL) inayochapisha gazeti la kila siku  la Kiswahili la UHURU na toleo lake la Jumapili  la MZALENDO na People’s Communication Media  inayomiliki Redio UHURU, CCM inatarajia kuwa televisheni mwezi February 2018.

Historia ya CCM kumiliki vyombo vya habari inaanzia  7 Julai 1954 wakati TANU ilipoundwa  na mara tu baada ya hapo ilianzisha gazette lake  la SAUTI YA TANU lililokuwa linashauriwa na rais wa chama Mwalimu Nyerere  ambaye baada  ya uhuru  alikuwa Rais wa Kwanza na Baba wa Taifa. 

TANU ilijaribu  kuanzisha gazeti la ligha  ya Kiingereza , National Times  mwaka 1959 ili kutaka sauti yake isikike kwa wasioongea Kiswahili  nchini. Hata hivyo hakukuwa na mtaji wa kutosha kwa ajili ya mradi huo na hivyo  kuahirisha. Hata  hivyo TANU ilidhamiria  kuwa na magazeti ya   Kiswahili na Kiingereza . Kwa hiyo siku ya Uhuru 9 Desemba1961, TANU ilizindua UHURU gazeti la wiki na baadaye la kila siku. UHURU limekuwa mbadala wa SAUTI  YA TANU . tarehe 30 Aprili, 1972, TANU ilizindua MZALENDO , kuwa   toleo la  Jumapili la UHURU. TANU ilianzisha gazeti la Kiingereza la Nationalist tarehe 17 April 1967 la kila wiki halafu   kila siku. TANU iliunganisha The Nationalist NA  The Standard  - Tanzania  5, Februari  1970 baada ya kubinafsisha  gazeti binafsi.  Tanganyika Broadcasting Corporation iliyokuwa na muundo wa kikoloni nayo ili binafsishwa  1 Julai 1965 na kutwa Radio Tanzania Dar Es Salaa na kwa “Sauti “ya Serikali ya TANU.

Kwa hiyo  hadi 1970, TANU  ilikuwa na vyombo  vya habari vilivyodhamiria kutimiza lengo  lake  kuwaunganisha watu katika   ujenzi wa taifa . Hata hivyo, hakukuwa a sera rasmi ya vyombo vya habari baada ya Uhuru zaidi ya TANU na Serikali yake  kutumia vyombo vya habari  kuimarisha umoja wa kitaifa na kujenga taifa. Ilikuwa baada  ya kuzindua  Azimio la Arusha  5 Februari  1967, na ushawishi wa TANU uliyoenea, baadaye CCM kwenye vyombo  vya habari imetoa athari kubwa  TANU  iliandaa Semina za mara  mbili kwa mwaka, zilizohudhuriwa na watumishi  waandamizi  wa vyombo vya habari nchini na kupanga hatua zaidi za kuchukuliwa . Mwisho wa hatua hiyo kulikuwa miongozo elekezi ya sera yaliyoshwawishi utendaji  wa uandishi wa habari na maudhui. Baina ya semina za mara mbili kwa mwaka, TANU, kupitia wizara yenye  dhamana   habari na nafasi yao katika   ujamaa na kujenga  taifa. Utendaji  wa  vyombo vya habari  pia  ulishawishiwa na Kamati  Kamati ya Vyombo vya habari   ya TANU ambayo waziri mwenye dhamana  ya utangazaji alikuwa  mwenyekiti .. Kamati  hiyo ilikuwa na wajumbe   wane wa Kamati  kuu ya chama, wahariri watendaji wa magazeti ya Serikali  na ya Chama, Mkurugenzi na mhariri mkuu wa habari wa Redio Tanzania  Dar Es Salaam . Katibu  WA Kamati alikuwa Katibu mkuu wa Wizara  yenye dhamana ya habari. 

Waraka wa Rais, aliyoutoa Rais Nyerere  kutokana na wadhifa  wake  kama mhariri Mkuu  tarehe 5 February, 1970 wakati alipotaifisha  The Standard Tanzania, imeshawishi  kwa  kiasi kikubwa utendaji wa vyombo vya  habari  na maudhui. Ingawa  waraka huo  ulilenga  gazeti moja tu  mahususi, kanuni zilizowekwa na miongozo elekezi iliyotolewa  ilieleweka kuwa  ni sera ya vyombo vya habari  kwa sababu  imetaja vyombo vya habari vya umma  nchini kama chombo cha   utumishi wa umma. Inatosha kusema kuwa vyombo vya habari  nchini Tanzania  wakati wa mfumo wa  Chama  vilikuwa katika udhibiti mkali  wa TANU  na baadaye CCM . Tangu kurudishwa  tena kwa  mfumo wa vyama  vingi nya siasa 1992, ushawishi wa CCM kwa vyombo  vya habari  umekuwa si wa moja kwa moja  kupitia sheria  ambazo Serikali yake  imezitunga na maagizo yasiyo andikwa. 

Kampuni ya vyombo vya Habari
Aina za vyombo vya habari
  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ