Ijumaa
Ijumaa ni miongoni mwa magazeti sita ya Kiswahili yanayoandika habari za jamii za kusisimua na huchapishwa na kampuni ya Global Publishers & General Enterprises Limited. Mengine ni Risasi, Uwazi, Amani,Championi na Spotixtra. Kwa mujibu wa African Media Barometer - Tanzania (2008), Global Publishers Limited inamiliki magazeti matano ya habari za jamii za udaku na za kusisimua. Kutokana na hali hiyo, Ijumaa inalenga zaidi watu mashuhuri, hadithi fupi, burudani, michezo, umbeya na kiasi kidogo zaidi kuhusu siasa.
Kwa mujibu wa utafiti wa GeoPoll kuhusu usomaji wa magazeti, uliyogharimiwa na MCT (Aug/Sep 2018), Gazeti la Ijumaa ni miongoni mwa magazeti 10 yenye mtazamo wa kijamii na kisiasa (XX.XXX% ya wasomaji)
Kulingana na TCRA (2018), Global Publishers & General Enterprises Limited yenye magazeti sita, likiwemo Ijumaa, yanamilikiwa na Joachim Lusana Buyobe (100%). Pia anamiliki Geita online TV kwa 100%.
Naye Eric James Shigongo anaonesha kuhusika kwa karibu na kampuni. Anatajwa kuwa ni Ofisa Mtendaji Mkuu, Mkurugenzi na Msimamizi wa Global Group – na wakati mwingine kuwa ni mmiliki wa tovuti nyingi. Pia huwa anaitaja kampuni kwenye facebook yake. Nafasi yake haifahamiki kwa sababu wasifu wa Kampuni yake haukupatikana kwenye Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) na kampuni hiyo haikujibu maswali ya mahojiano.
Isa za hadhira
Aina ya umiliki
binafsi
Maeneo yanayofikiwa
taifa (mainland)
Aina ya maudhui
Maudhui yaliyolipiwa
Kampuni ya vyombo vya Habari
Global Publishers & General Enterprises Limited
Muundo wa umiliki
Ijumaa inachapishwa na Global Publishers & General Enterprises Limited, inayohusishwa na Eric Shidongo.
Haki ya kuchagua
Taarifa zisizopatikana
Kundi / Mmiliki Binafsi
Joachim Lusana Buyobe
Raia wa Tanzania hajionyeshi. Pia anamiliki Geita online TV kwa 100%.
Maelezo yote
Mwaka wa kuanzishwa
1998
Mwanzilishi
Abdallah Mrisho Salawi hakuna taarifa zaidi kuhusu mwasisi mwenza. Eric Shigongo - ni mjasiriamali, mwandishi wa vitabu na msemaji. Alizaliwa Mwanza, kwenye fukwe za ziwa Victoria, ana kampuni mbalimbali zikiwemo vyombo vya habari, hoteli, kilimo, uendel
Mtendaji Mkuu
Taarifa zisizopatikana
Mhariri Mkuu
Taarifa zisizopatikana
Watu wengine muhimu
Taarifa zisizopatikana
Mawasiliano
Global Publishers & General Enterprises Limited
P. O. Box 7534, Dar-Es-Salaam
Tel.:
E-Mail:
Taarifa za kifedha
Taarifa ya Kifedha
Taarifa zisizopatikana
Faida za uendeshaji
Taarifa zisizopatikana
Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)
Taarifa zisizopatikana
Isa katika soko
Taarifa zisizopatikana
Maelezo ya ziada
Taarifa ya ziada
Kwa mujibu wa utafiti wa GeoPoll (Agost 30 – 1 Sep 2018), kuhusu hadira uliyodhaminiwa na MOM Tanzania. Magazeti yenye maslahi maalumu kama vile habari za michezo hayakujumuishwa kwenye uchambuzi wa umiliki.