This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/04/19 at 03:49
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Clouds TV

Ilizinduliwa mwaka 2010 kama kituo cha TV cha binafsi jijini Dar es salaam na inamilikiwa na Clouds Media Group inayoendesha pia Clouds Redio, Coconut FM na Choice FM. Ni ya nne miongoni mwa vituo vya TV vinavyoangaliwa sana nchini Tanzania yenye XX.XXX% ya hadhira kwa mujibu wa utafiti wa GeoPoll wa robo ya pili ya mwaka.

Ni kituo chenye vipindi vya vijana na ndivyo vilivyofanya kuwa Clouds TV kuwa TV nambari moja katika kipengele cha vijana na kituo cha kwana kuunganishwa kwa ukamilifu na mitandao ya kijamii na kushirikishwa na kila inapotangaza.

Mchanganyiko wa vipindi vya tamthilia zilizotengenezwa nchini na sinema za mapenzi na za matukio halisi na kuchanganya na habari za matukio makubwa na vipindi vilivyotayarishwa kwa uchambuzi wa kina kuhusu mitindo ya maisha imefanya kituo kipendwe zaidi na vijana ambao ni 60% ya Watanzania.

Licha ya habari na matukio, kituo hiki pia kinatangaza vipindi vya aina mbalimbali, kuanzia miziki mbalimbali, vipindi maalumu mijadala na habari za burudani, sinema za mapenzi, burudani na michezo.

Kituo hiki kinamilikiwa na Clouds Media Group ambapo Joseph Kusaga, mjasiriamali maarufu na mwasisi mwenza, ni mtendaji mkuu. Kusaga alianza kama DJ na alifanya matamasha na disko nchini kote Tanzania kabla ya kuanzisha kwa ubia C.L.O.U.D.S (Cool, lovable, Outrageous, Unique, Sound) FM. Tangu kuanzishwa kwa Clouds, Kusaga ameendelea kujenga kampuni za vyombo vya habari vyenye mafanikio, ukarimu na teknolojia.

Taarifa kuhusu Clouds Media Group si rahisi kupatikana; Kampuni hii haikusajiliwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), wala namba yake ya uandikishaji ili kupata wasifu wa kampuni katika Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).

Taarifa muhimu

Isa za hadhira

Aina ya umiliki

Binafsi

Maeneo yanayofikiwa

Taifa

Aina ya maudhui

Free to Air

Taarifa zinazopatikana kiurahisi

Upatikanaji wa taarifa za umiliki kutoka kwa vyanzo vingine, kwa mfano vile vinavyotambulikana kisheria

2 ♥

Kampuni ya vyombo vya Habari

Clouds Entertainment Co. Limited

Umiliki

Muundo wa umiliki

Clouds Television Limitedni ya kwanza miongoni mwa vituo vya TV na kumilikiwa na Clouds Entertainment Limited, ambayo ni mali ya Kusaga na familia yake. Kwa mujibu wa data za TCRA na BRELA.

Haki ya kuchagua

Taarifa zisizopatikana

Mmiliki Binafsi

Kundi / Mmiliki Binafsi

Alex Mkama Kusaga

ni baba mzazi wa Joseph Kusaga, muasisi wa Clouds Entertainment Limited. Amefariki Afrika Kusini mwaka 2009 na alizikwa Dar es Salaam 7t Novemba 2009. Hadi 2018, bado ameorodheshwa kuwa mmiliki wa hisa.

25%
Kampuni ya vyombo vya Habari
Halisia

Maelezo yote

Mwaka wa kuanzishwa

2010

Mwanzilishi

Joseph Kusaga - alipenda muziki tangu mdogo. alianza kuendesha matamasha tangu akiwa chuoni akisomea elektoniki, akiwa DJ maarufu na mtayarishaji matamasha. Alipata wazo la kuanzisha kampuni ya vyombo vya habari wakati alipotembelea USA, alipoungana na m

Mtendaji Mkuu

Joseph Kusaga - angalia hapo juu

Mhariri Mkuu

Ruge Mutabaha - Mkurugenzi wa Vipindi

Mawasiliano

Clouds Media Group

P.O: Box 311513, Dar-Es-Salaam;

Tel.: +255222781445

E-Mail: info@cloudsmedia.co.tz

www.cloudsmedia.com

Taarifa za kifedha

Taarifa ya Kifedha

Taarifa zisizopatikana

Faida za uendeshaji

Taarifa zisizopatikana

Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)

Taarifa zisizopatikana

Isa katika soko

Taarifa zisizopatikana

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ