This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/04/20 at 13:32
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Clouds Entertainment Co. Limited

Clouds Entertainment Co. Limited

Clouds Media Group ni kampuni ya kimataifa na vyombo vya habari mbali mbali na miongoni mwa vyombo vya habari vinavyoongoza katika Afrika Mashariki na kati. Clouds inatetea zaidi sauti inayobadilika, tulivu, inayopendwa, yenye nguvu na ya kipekee (cool, lovable, outrageus, unique, Dynamic, sound), ilianzishwa mwaka 1998 na Joseph Kusaga na Ruge Mutahaba.

Akivutiwa na mandhari ya muziki ya Los Angeles, Kusaga ameungana na mdau wake wa biashara wa muda mrefu, Ruge Mutahaba, walianza kupanga kituo cha redio kwa Tanzania ambacho muda si mrefu kitakuwa Clouds FM. Ilianza na kituo kimoja cha redio chenye chumba kidogo cha Studio. Kuanzia hapo, Clouds imekuwa na kuchanua na kuwa Shirika linaloshughulikia vyombo vyote vya utangazaji kwenye nyanja za usimamizi wa matukio, masoko na dijiti.

Hivi sasa kampuni hiyo inaendesha vituo vya redio; Clouds FM inayojulikana kuwa “Redio ya Watu”, Choice FM kituo cha burudani cha Kiingereza kwa ajili ya wataalamu vijana wa Tanzania waliosoma nchi za nje na sasa wamerudi nchini na coconut FM inayotangaza kutokea Zanzibar.

Kampuni ya Clouds inamiliki vituo tisa vya TV, ikiwemo Clouds TV, 50- Channel cable. DTT TV Network, OTT platform, kampuni ya masoko ya matukio, Ngoma web TV na Gazeti la Kitangoma. Hasa Clouds FM na Clouds TV siku hizi ni vyombo vya habari vinavyosikilizwa na kutazamwa zaidi nchini. Kampuni hii yenye zaidi ya wafanyakazi 300 ina hadhira kubwa Afrika Mashariki na Kati, Mashariki ya Kati na Visiwa vya Caribbean na kufungwa Ofisi Kingston Jamaica.

Hakuna data za Kampuni katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Kuna wasifu wa kampuni kwa ajili ya Clouds Television katika Wakala ya Usajili wa Biashara na Utoaji wa Leseni (BRELLA), kwa mujibu wa taarifa hizo, Alex Mkama anamiliki hisa 25% kama Joseph Kusaga. Clouds Entertainment Limited inamiliki 50% ya hisa.

Ruge Mutahaba hivi sasa bado ni Director of Strategy and Programs Development katika Clouds Media Group.

Taarifa muhimu

Aina ya Biashara

Umma

Mfumo kisheria

Binafsi

Nyanja za Kibiashara

Utangazaji, Matangazo ya biashara

Umiliki

Mmiliki Binafsi

Joseph M. Kusaga

Joseph Kusaga - Mkurugenzi Mtendaji. alizaliwa mwaka 1966, Mtanzania. alipenda muziki tangu mdogo. alianza kuendesha matamasha tangu akiwa chuoni akisomea elektoniki, akiwa DJ maarufu na mtayarishaji matamasha.
Alipata wazo la kuanzisha kampuni ya vyombo vya habari wakati alipotembelea USA, alipoungana na mbia wake wa biashara wa muda mrefu Ruge Mutahaba, na kuanzisha mpango wa kituo cha redio kwa Tanzania ambacho baadae kitakuwa Clouds FM.

50%

Judith Violet Kusaga

Mkurugenzi. Amezaaliwa 1955. Mtanzania.

10%
Vyombo vya habari
Other Media Outlets

Televisheni zingine

Clouds TV

Radio nyingine

Clouds FM

Halisia

Chombo cha habari cha kibiashara

Utangazaji

Clouds Television Limited

Biashara

hakuna

Cloud broadcasts in Rwanda.

Maelezo yote

Mwaka wa kuanzishwa

1998

Mwanzilishi

Joseph Kusaga - developed a passion for music at a very early age. He started to organize events when he was still at the college studying electronics, and became a very popular DJ and event organizer.
He got the idea to start a media company during his visit to the USA, where he connected with his life-long business partner, Ruge Mutabaha, and started to plan a radio station for Tanzania that would later become Clouds FM.
Alex Mkama Kusaga - passed away. Father to Joseph Kusaga.

Waajiriwa

Taarifa zisizopatikana

Mawasiliano

Clouds Media Group

P.O: Box 311513, Dar-Es-Salaam;

Tel.: +255222781445

E-Mail: info@cloudsmedia.co.tz

www.cloudsmedia.com

Namba ya kutambulika

BRELA incorporation n°: 30218

Taarifa za kifedha

Taarifa ya Kifedha

Taarifa zisizopatikana

Faida za uendeshaji

Taarifa zisizopatikana

Utangazaji(jumla ya mapato kwa asilimia)

Taarifa zisizopatikana

Utawala

Bodi ya utendaji + Bodi Maslahi ya utendaji

Manase Simon Gillar

Company Secretary as of 2016.

Bodi isiyo ya utendaji + Bodi maslahi isiyo ya utendaji

All owners are also registered as company directors.

Watu muhimu wenye ushawishi + watu maslahi wengine muhimu

Ruge - Director of Strategy and Programs Development at Clouds Media Group in Tanzania.

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ