This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-gmr.org/en/ retrieved on 2024/04/20 at 09:49
Global Media Registry (GMR) & Media Council of Tanzania - all rights reserved, published under Creative Commons Attribution-NoDerivatives 4.0 International License.
Media Council of Tanzania LOGO
Global Media Registry

Dr. Anthony Diallo

Dr. Anthony Diallo

Dkt. Anthony Diallo, ni mwanasiasa na mbuge wa zamani, ni mwasisi wa Sahara Media Group Limited, kampuni ya vyombo vya habari inayoendesha Star TV, Radio Free Africa na Kiss FM, na makao yake jijini Mwanza. Hakuna data za umiliki wa Sahara Media Group kwenye Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), tovuti nyingi zinamtaja Diallo kuwa ni Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo.

Dkt. Diallo, ambaye hivi sasa ni Mwenyekiti wa Chama Tawala cha Mapinduzi CCM) wa Mkoa wa Mwanza alikuwa mbunge anayewakilisha jimbo la Ilemela mkoani Mwanza kuanzia mwaka 1995 hadi Oktoba 2010, alipopoteza kiti hicho kwa mgombea wa Chama cha Upinzani cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Ametumikia nyadhifa mbalimbali katika baraza la mawaziri kuanzia mwaka 2000 hadi 2008. Alikuwa naibu wa Waziri wa Biashara na Viwanda, Naibu Waziri wa Maji na Mifugo na Waziri wa Maliasili na Utalii.

Dkt. Diallo anashughulikia biashara-mtandao (e-Business), Serikali-mtandao (e-Government) na utekelezaji wa mifumo. Ana uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika Nyanja za utengenezaji bidhaa, ununuzi na kupanga uzalishaji.

Kabla ya kujiunga kwenye biashara ya vyombo vya habari, mwaka 1992, Dkt Diallo alikuwa mwasisi mwenza wa DM investment Co. Ltd, miongoni mwa kampuni kubwa zaidi za uhandisi na utengenezaji bidhaa nchini.

Kampuni iliyofungwa mwaka 1994 ilitengeneza Bidhaa za Sahara za vyombo vya umeme, mashine za kilimo, injini za dizeli za “single stroke” na mitambo ya viwandani kwa ajili ya viwanda vya uchakataji wa bidhaa za kilimo.

Dkt Diallo alizaliwa 25 Desemba, 1956 ana shahada ya kwanza ya Sayansi (BS – eB) katika biashara mtandao (e-Business) kutoka Chuo Kikuu cha Phoenix, Shahada ya Uzamili ya Usimamizi wa Biashara (MBA) kutoka Chuo Kikuu cha NewCastle, Shahada ya Uzamili ya Usimamizi wa Kitaifa kutoka Chuo Kikuu cha Phoenix (MM-I), na Shahada ya Uzamivu katika Usimamizi wa Biashara (BDA) kutoka Chuo Kikuu cha NewCastle (2008).

Pia ana stashada ya Uzamili katika Usimamizi wa Teknolojia kutoka Maastricht School of Management, NL na Mhitimu wa Advanced Management Program wa Harvard Business School, Boston, USA (1994).

Kampuni ya vyombo vya Habari
Aina za vyombo vya habari
Halisia

Biashara

HISTORIA YA AJIRA

DM Investments

Managing Director: 1992

General Health

Sales Officer: 1978

Mwanza Chemist

Managing Director: 1973 - 1975

Mwananchi Dispensary

Dispensary Assistant: 1971 1972

Roman Catholic

Mission Clerk: 1969

Ministry of Livestock Development

Minister 10/17/2006 - 2/8/2008

Ministry of Natural Resources and Tourism

Minister 1/1/2006 - 10/16/2006

Ministry of Water and Livestock

Deputy Minister: 2001 - 2005

Ministry of Industry and Trade

Deputy Minister: 2000 - 2000

Chama Cha Mapinduzi (CCM)

District Political Committee Member 1995 To Date

Parliament of Tanzania

Member of Parliament of Tanzania: 1995 - 2010

  • Project by
    Media Council of Tanzania
  •  
    Global Media Registry
  • Funded by
    BMZ